Friday, November 28, 2014

Waigizaji wa kiafrika, Kizungu na vimbwa


                                                                




Waigizaji wengi wa Afrika wanapenda kuiga mambo ya  Ulaya na Marekani.  Kwa  vile mastaa  wengi wa Ulaya na Marekani wanapenda kutembea na vimbwa,  hivi sasa kila  anayejiona staa anatembea na kiumbe. Vipo vitu vya kuiga sio kutembea na viumbwa.  Tuwe makini  na mambo tunayoiga. Mastaa wengi wa Ulaya na Marekani  wanatafuta vimbwa kwa ajili ya kujifurahisha kimapenzi,  hayo yaliwekwa na  mwandishi mmoja wa habari za kijamii nchini Marekani, Josephine Cris aliandika mtandaoni kuwa, mchezo huo uko sehemu nyingi ulimwenguni licha ya kwamba una madhara. “Mara nyingi wanawake wengi wanatumia mbwa kujifurahisha katika mapenzi,  kwa sababu wanauwezo mkubwa kutumia ulimi kulamba kitu bila ya kuchoka. Wengi hufanya hivyo kwa siri kwani wanajua jamii itawashangaa kama watasikia taarifa zao.  Ni vitendo vinavyochukiza  sana hasa ukichukulia kwamba madhara ya kufanya mapenzi na mbwa yapo wazi. Hebu jiulize, kipi kinachoweza kukuvutia kwa mbwa hadi akupe mshawasha wa kufanya naye mapenzi, kwanza mnyama siku zote ni mchafu na anaweza kukuambukiza maradhi, sasa sijui kwa nini watu wanawatumia kimahaba,” anaeleza Josephine. Kwa upande wa waigizaji wa Afrika, hatujui kama wanahusika au ni kuiga bila ya kujua wanachoiga. Tuwe makini na vyakuiga sio kila kitu tunaiga.

Maajabu makubwa, binti amefunga ndoa na mbwa

.
                                                         Kufundoa na mbwa

Binti amefunga ndoa  na mbwa kwa ajili ya kuondoa mikosi na majanga  ya kimaisha, harusi hiyo imefanyika hadharani bila ya kuficho chochote. Wazazi wa mwanamke wafurahia kama vile binti yao ameolewa na mtoto wa tajiri namba moja duniani. Hebu niambie duniani inaelekea wapi?  Tutafakari na kumrudia mungu  wangu kwa kufanya ibada ya kweli na sio ibada za kinafiki. Hatuwezi kujua lini duniani itafika mwisho kama vitabu vya dini vinavyosema.

Chike Ike akitesa Dubai kwa raha zake, Mambo ya fedha








                                                             Chike Ike kwenye boti
                                                           Chike Ike akiburudika na kahawa
                                                          Chike Ike akipata mchana mwema
                                                               wakiwa ndani bori
                                                    Chike akiwa kwenye fukwe
                                                           Chike akiwa kwe boti


Marehemu Marijani Rajabu aliyekuwa  mwanamuzki wa Dar Intenatinal aliwahi kuimba pesa ni sabuni ya roho. Mwenye pesa akifika watu wote wanasimama kila analosema watu wanalipa uzito hata kama ni wazo la kijinga.  Ndiyo ilivyokuwa kwa muigizaji wa Nigeria, Chika Ike akitumia fedha anavyotaka katika  fukwe ya jiji  Dubai ambapo unaambiwa alikodi  boat kwa dola elfu 24,000 kwa muda wa siku mbili tu,  na kila alilosema alisikilizwa na lilitekelezwa kwa kasi ya ajabu.  PESA ni  mfalme wa dunia,  ukibisha wewe bisha lakini ndio ukweli wenyewe.

Thursday, October 30, 2014

Mwandishi yafichua machafu ya watu



Wapenzi wa kazi za Haji Dilunga, tarajieni kupata sinema  nyingine ya Mwandishi wa habari. Script nimeandika katika ubora wa hali ya juu, Kama uliburudika na Kwanini Mama  sambamba Jamila na Pete ya Ajabu. Mwandishi ni zaidi ya kile unachofikiria. Ni sinema aliyotumia  muda mwingi kufanya utafiti wa namna ya fani ya habari inavyotumika kwa faida ya wajanja wachache. Ni ujanja gani? Na nani anafanya ujanja huo ni kuitafuta DVD ya sinema  iliyoingia hivi karibuni. Imetayarisha na Kampuni ya Big One Entertainment. Daima ubora kwanza. Kama kawaida imeatungwa nakuandikwa na Haji Dilunga

Kwanini Mama yatoa wengi machozi



Kwanini mama ni sinema inayozungumzia maisha ya watoto wa kiume wanavyowanyanyasa mama zao na kuwasikiliza wake zao. ni sinema yenye mafunzo ya hali ya juu sio vizuri kuikosa. Stori na script ni kazi ya Haji Dilunga.



Jamila bado inatesa sokoni

Ile sinema ya Jamila na pete ya ajabu bado inaendelea kuvutia wengine,kila kukicha wapenzi na mashabiki wamekuwa wakiizungumzia. Ni sinema inayozungumzia unyanyasaji wa watoto. Imetungwa na Haji Dilunga.


                                                           Jamila akicheza na nyani
                                                              Jamila akicheza nyani
                                                    Jamila akipanda ngamia
                                                       Jamila akiwa juu ya ngamia

Thursday, October 10, 2013

Sound of Soul itakuwa mitaani hivi karibuni


Sinema ni sanaa ya maigizo kwa njia ya vitendo, inayoelimisha jamii kwa mfumo wa picha. Lengo la mtayarishaji kutengeneza sinema ni kutaka kufikisha ujumbe kwa jamii iliyotuzunguka.
Wataalamu wa sanaa ya sinema, wamebainisha kwamba sinema imegawanyika katika makundi tofauti, kuna sinema zinazohusu maisha ya mtu fulani au famila. Sinema nyingine zinahusu jamii husika, mfano sinema ya Sound of Soul, inaelezea madhara ya tamaa katika jamii yetu ya kitanzania.
Kwa mujibu wa maelezo ya msemaji wa kampuni ya Swahili World Picture, Haji Dilunga
ambaye ndiye mtunzi na mwandishi wa script hiyo, amesema kisa hicho kiliwahi
kutokea miaka ya nyuma kabla ya yeye (Dilunga) hajazaliwa, baada ya kusimulia
aliamua kutayarisha sinema ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hiyo.
Dilunga ambaye ni mwandishi wa habari, amesema kisa hicho amekiboresha ili kiweze
kuwa na mvuto kwa watazamaji, pamoja na kuongeza matukio ya kusikitisha na
kuhuzunisha.
Amesema sinema hiyo inamzungumzia msichana Whitney, aliyekuwa na tamaa ya kutafuta
mali baada ya mali za urithi alizoachiwa na marehemu baba yake, kunyang'wa na Baba
yake mkubwa, alipokuwa na mdogo na hatimaye kufukuzwa kwenye nyumba yao pamoja na
mama yake.
Kitendo hicho kilimfanya Whitney kutafuta mali kwa udi na uvumba, ili aweze kuwa
na maisha mazuri. Kwa bahati nzuri alifanikiwa kuwa na maisha mazuri, baada ya
muda mfupi maisha mazuri yalimtumbukia nyongo.
Ni nani aliyesababisha maisha mazuri yamtumbukie nyonge, ni msichana mwingine
anayeitwa Lolita, Msichana huyu alitokea kumsumbua Whitney kupita kiasi. Nini
matokeo ya usumbufu wa Lolita kwa Whitney? Unajua kwanini alimsumbua? Jibu
utalipata baada ya kuangalia Sound of Soul.
Utamu wa sinema hiyo unakuja pale unapotaka kujua kama sio kufahamu, kilichompata
Baba yake mkubwa Whitney, baada ya kumnyang'anya mali Whitney. Alifanikiwa kutimia
mali hizo, au alizikimbia na kuchukuliwa na watu wengine? Ukibahatika kuangalia
Sound of Soul utafahamu kisa hicho cha kusisimua.
“Nadhani wale wanaofuatilia sinema ninazotengeneza, watakubaliana na mimi kwamba si bahatishi katika utunzi na uandishi wa script sambamba na kuidirect movie. Watakumbuka sinema zangu nilizoandika script na kudirect ni pamoja na Uwanja wa dhambi, I love you, Picnic, Bunge la Wachawi, Popobawa na Zindiko." Alisema Dilunga.
Sound of Soul inawataka vijana kutafuta mali au fedha kwa njia ya halali, pia wanatakiwa kufahamu kama umauti pia upo nyuma yetu. Kutafuta fedha au mali kwa njia zisizokubali na jamii yetu au muumba wetu, nikujitafutia matatizo katika maisha yako ya duniani na kesho ahera.

“Sisi ni tofauti na watengenezaji wengine wa sinema, sisi hatutengenezi sinema zenye visa vya mapenzi ya kufikirika. Tunatengeneza sinema zenye ujumbe wa visa vya kweli katika maisha ya binadamu." Alisema Dilunga.
Amesema Sinema kama uwanja wa dhambi ilivuma sana, mpaka leo bado watu wanaikumbuka. Kuna baadhi ya wapenzi wa sinema walitoka Mombasa kuja kuonana na waigizaji wa sinema ya uwanja wa dhambi.
“Hebu fikiri watu wamefunga safari toka Mombasa kuja Dar kuonana na waigizaji waliocheza uwanja wa dhambi, sio jambo la kawaida kutokea katika sanaa. Mara nyingi tumezoea kusikia na kuona watu wakitoka mikoani sio nje ya nchi." Alisema Dilunga.
Amesema Sound of Soul ni sinema nzuri inayofaa kuangalia na familia yako, kwa sababu imezingatia maadili ya kitanzania. Hakuna mwigizaji yoyote aliyevaa nguo za ajabu kama nusu uchi, unaweza kuangalia na watoto wako bila ya kujisikia vibaya.
Sinema hiyo imechezwa na Mwajuma Abdul Haji, aliyecheza kama Whitney. Fatuma Mwinchumu amecheza Mama Whitney, Jimmy Raphael amecheza kama Baba mkubwa. Nurati Ngereshi amecheza kama Lolita.
Wengine waliocheza majina ya kiuchezaji yakiwa kwenye mabano ni Zalka Athumani (Rose),Emilio John (Mganga Puchiro),Sikudhani Mkambo( Mke wa Puchiro), Clemencea Salum (Tina), Khadija Fundi(Bi Upupu), Peter Pascal (Mganga Chanuo),Apolinary Mathew(Bonzo) Abdullah Hassani (Bwino), Paul Leonard(Meneja), Amina Omary (Polisi), Paskazia Peter(Polisi), Halima(Magret),Yusuph (Polisi) na Said (Polisi)
Sound of Soul inatarajia kuingia sokoni mara baada ya kumalizika kueditiwa, kuna scene kama tatu zinafanyiwa marekebisho kwa ajili ya kuwapatia wapenzi uhondo wa aina yake.
Kwa wale vijana wanaotaka kuendeleza vipaji vyao, wanaweza kufika ukumbi wa CCM tawi la Amani siku ya jumanne, alhamisi na jumamosi saa kumi jioni. Au  wanaweza kupiga simu namba 0789 904 226 au 0657 675 531.